Thursday, March 21, 2013

Prince Boateng atoa hotuba kali UN kuhusu ubaguzi

Boateng akisoma hotuba yake UN

Kiungo wa Ac Milan Kevin Prince Boateng leo ametoa hotuba yenye hisia kali kwenye kikao cha Umoja wa Mataifa (UN) katika kuadhimisha siku ya kupinga na kutokomeza ubaguzi. Boateng alikwenda kutoa hotuba hiyo ikiwa ni siku chache baada ya kufanyia kitendo cha kibaguzi na mashabiki wa timu ya Pro Patria wakati Ac Milan  ilipokuwa ikicheza mechi ya kirafiki. Katika tukio hilo Boateng alitoka nje ya kiwanja kwa hasira na kukiomba chama cha soka nchi Italia kuchukua hatua kwa kitendo hicho. Katika hotuba hiyo ambayo imewagusa wengi, Boateng amesema “Ubaguzi ni kirusi hatari kisichokuwa na faida ambacho kimeadhiri watu wengi. Katika kikao hicho Kevin aliongeza kwa kusema, ataendelea kuwa balozi wa vita dhidi ya ubaguzi na atajitahidi akutane na Rais wa FIFA Sepp Blatter ili aweze kumpatia mawazo ya kupigana na ubaguzi hasa kwenye mchezo wa soka.

No comments:

Post a Comment