Thursday, March 21, 2013

Rais Kikwete azindua Azam Complex


Rais Jakaya Kikwete, leo mchana amezidua uwanja wa Azam Complex unaomilikiwa na klabu ya Azam FC, Chamazi, Mbande, Dar es Salaam. Azam iliyopo chini ya kampuni ya Bahressa Group ndiyo club ya kwanza nchini Tanzania kumiliki uwanja ambao unaweza kutumika kwa ajili ya mechi za ligi na michezo mingine. 


Raisi Kikwete amezindua uwanja huo ambao tayari ulishaanza kutumika kwa mechi za Ligi Kuu Bara na michezo mingine tangu msimu wa mwaka 2011 chini ya Mkurugenzi Mkuu, Aboubakary Bahkresa. Uwanja huo ambao bado upo kwenye hatua mbalimbali za kuendelezwa zaidi unauwezo wa kubeba watazamaji 7,000 kati yao 700 ni VIP.  

No comments:

Post a Comment