Thursday, April 11, 2013

Ligi kuu England kutumia "Goal line technology"

Shirikisho la soka nchini Uingereza leo kimethibitisha matumizi ya tekinologia ya kutambua goli “goal line technology” ambayo itaanza kutumika kuanzia msimu ujao wa ligi. Maamuzi ya matumizi ya teknologia hii yamefikiwa baada ya FA kufanya kikao na viongozi wa timu zote 20 za ligi hiyo na kukubaliana. Kampuni moja ya Kiingereza ndiyo imeshinda tenda hiyo ambapo itafunga kamera saba kwenye kila goli na gharama ya kufunga teknologia hiyo kwenye kila kiwanja ni paundi 250,000 sawa na tsh mil 605. FA imesema teknologia hiyo itatumika kwenye viwanja vya ligi kuu tu, viwanja vingine vitafungiwa teknologia hiyo miaka ijayo kwasababu gharama zake ni kubwa.


Saa atakayoivaa refa ambayo itamjulisha kama ni goli au sio goli, ikiwa goli limeingia itaonesha "Goal", kama goli halijaingia haitaonesha kitu. Saa hii atavaa mwamuzi wa kati, wa pembeni na waamuzi wa akiba
Wakati FA wakianza kutumia teknologia hiyo shirikisho la mpira wa miguu nchini Hispania limesema, Hispania itaanza kutumia teknologia hiyo baada ya miaka mitatu ijayo licha ya FIFA kuruhusu matumizi ya teknoligia hiyo kuanza kutumika duniani kote. FIFA itaanza kutumia teknologia hiyo mwaka 2014 katika michuano ya kombe la dunia nchini Brazil ikiwa ni majaribio ya matumizi ya teknologia hiyo. 

Goli lililokataliwa la Lampard kwenye kombe la dunia Afrika ya Kusini katika mechi kati ya Uingereza na Ujerumani. Mwamuzi alikataa goli hili kwasababu halikuvuka mstari wa kati, lakini televisheni zilionesha mpira huo ulivuka mstari wa kati
Mjadala wa teknologia ya kutambua goli ulipamba moto kwenye michuano ya kombe la dunia nchini Afrika kusini katika mechi kati ya Ujerumani na Uingereza baada ya refa kukataa goli lililofungwa na Frank Lampard kwa madai kuwa hakuona kama limevuka mstari. Tukio hilo ndilo liliamsha mjadala wa matumizi ya teknologia ya goli ambao umeshabikiwa sana na chama cha mpira nchini Uingereza ili iweze kutumika, na uamuzi wa FA kuanza kutumia teknologia hii ni moja ya jitihada za FA kuishawishi FIFA na wanachama wake kuitambua na kuanza kuitumia jambo ambalo linaonesha kufanikiwa. 

No comments:

Post a Comment