Thursday, April 11, 2013

Yanga imegoma kuonekana Supersport

Uongozi wa klabu ya Yanga imegoma mabadiliko ya ratiba ya ligi kuu Tanzania bara na kuoneshwa kwa mechi zake na kituo cha televisheni DSTV kupitia chaneli yake ya Supersport. Yanga katika barua yake iliyopeleka kwenye uongozi wa TFF imesema  haipo tayari kwa mabadiliko hayo ya ratiba, kwani klabu imeshatumia gharama nyingi kuiandaa timu na kusogezwa mbele kwa michezo ni kuwaongezea gharama za uendeshaji wa timu. Pili klabu ya Yanga ilisikitishwa na Kamati ya Ligi na TFF kufikia makubaliano na kituo hicho cha Luninga pasipo kuishirikisha timu ya Yanga ambao ndio haswa walengwa wa mchezo huo, kwani mpaka sasa Yanga hawajui klabu itafaidika vipi na matangazo hayo. Mbali ya Yanga kuandika barua hiyo lakini TFF na Kamati ya Ligi bado hawajajibu barua hiyo mpaka sasa. Msimamo wa klabu ya Yanga ni kuwa haitakubali kampuni ya DSTV kupitia kituo chake cha Supersport kuonyesha michezo yake moja kwa moja bila ya kuongea na uongozi wa klabu ya Yanga. Hatua hii ya Yanga imekuja baada ya TFF kupangua ratiba ya mechi sita ili ziweze kuoneshwa moja kwa moja na kwenye luninga, kufuatia mabadiliko haya klabu nyingi zimeonesha kutokukubaliana na TFF ikiwemo klabu ya Yanga

No comments:

Post a Comment