Thursday, April 11, 2013

Tanzania imepanda kwenye renki za FIFA

Tanzania imependa kwa nafasi tatu kwenye viwango vya FIFA duniani. Tanzania iliyokuwa nafasi ya 119 imepanda hadi nafasi ya 116. FIFA imetoa matokeo hayo leo ambapo kupanda kwa Tanzania kumechangiwa kwa kiasi kikubwa na matokeo mazuri iliyoyapata kwenye mechi zake iliyocheza mwaka huu na kushinda dhidi ya Morocco na Cameroon. Tanzania imeweza kufikisha pointi 305 kutoka pointi 263 ilizokuwanazo awali. Kwa timu za Afrika, Tanzania imepanda hadi nafasi ya 33 ikiwa juu ya Kenya ambayo ipo nafasi ya 34. Kudhihirisha ubora wa Tanzania katika soka, Tanzania kwasasa ipo nafasi ya pili kwenye kundi lake la kuwania kufuzu kombe la dunia ikiwa na pointi sita tofauti ya pointi moja na vinara wa kundi hilo Ivory Coast wenye pointi saba, wakati timu ya Morocco inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi mbili na Gambia ni ya mwisho ikiwa na pointi moja. Katika kundi hilo, Tanzania ipo mbele kwa tofauti ya pointi nne dhidi ya Morocco, timu ambayo inashikilia nafasi ya 74 kwenye viwango vya FIFA ikiwa ni kiwango cha juu mara mbili zaidi ya Tanzania, vilevile Tanzania imetofautiana pointi moja tu na Ivory Coast, timu ambayo inashikilia nafasi ya 12 kwenye viwango vya FIFA duniani na nafasi ya kwanza kwa timu za Afrika. Kwa kuonesha ushindani huu kwa timu ambazo zimeidizi viwango ni dhahiri kiwango cha Tanzania kimekuwa kwa kiasi kikubwa sambamba na mchezo mzuri inayoonesha ikiwa kiwanjani. Katika matokeo yaliyotoka leo timu ya Brazil imeshuka hadi nafasi ya 19 wakati Hispania ikiwa nafasi ya kwanza, ikifuatiwa na Ujerumani nafasi ya pili na Ajentina nafasi ya tatu. 

No comments:

Post a Comment