Kocha wa Tottenham, Andre Villas-Boas ameiomba klabu yake
kuongeza mkataba na malipo ya Gareth Bale ili ajifunge zaidi kuitumikia klabu hiyo.
Mkataba wa sasa wa Bale unakwisha mwaka 2016 na malipo yake ni paundi 75,000 kwa wiki, lakini Villas Boas amehitaji
mchezaji huyo apewe mkataba wa miaka mitano na kuongezewa mshahara mara mbili
zaidi ya sasa. Villas-Boas katika maongezi yake amesema anahitaji Bale afanyiwe
hivyo kwasababu anacheza vizuri na kwa kiwango chake anastahili kulipwa kama
wachezaji wengine wakubwa duniani na vilevile itamfanya aipende zaidi Tottenham
na kumuondolea vishawishi vya kutaka kuhama kwenda kwenye vilabu vikubwa zaidi.
Bareth Bale mwenye umri wa miaka 23 kwasasa anahitajiwa na vilabu vingi duniani
ikiwemo Real Madrid, PSG na Man utd na dhamani yake kwasasa imeongezeka baada ya kupata tuzo ya mchezaji bora wa Uingereza nakufikia paundi mil 80 – 100 akimpiku mshambuliaji wa Santos Neymar mwenye dhamani ya paundi mil 45-60.
No comments:
Post a Comment