Sunday, May 12, 2013

Mancini kufukuzwa, Pellegrini kuchukua nafasi yake

Kocha wa Manchester City Roberto Mancini anatarajiwa kufukuzwa kazi wiki mbili zinazokuja na kumuachia nafasi hiyo kocha wa Malaga Manuel Pellegrini. Taarifa hizi zimetoka ndani ya uongozi wa Man city bila kutajwa majina ya waliotoa taarifa hizi kwasababu muda wa kutangaza rasmi bado haujafika. Likielezea swala hili, gazeti la Sportmail la Uingereza limesema Mancini aliwekewa malengo mawili mwaka huu ili aweze kuendelea kuwa kocha wa klabu hiyo. Lengo la kwanza lilikuwa, kutetea ubingwa wa ligi kuu na lengo la pili Mancini alitakiwa kuhakikisha Man city inafikia hatua ya robo fainali za klabu bingwa barani Ulaya (UEFA champions) malengo ambayo ameshindwa kuyatimiza. Kwa sababu hizi ndiyo maana uongozi wa Man city umeamua kumfukuza kazi  Mancini. Vilevile taarifa hizi zilisema hata kama Mancini angeweza kushinda FA bado alikuwa anafukuzwa kazi kwasababu kombe la FA halikuwepo kwenye malengo ya mwaka huu ya klabu ya Man city. Roberto Mancini (48) alijiunga na Man city mwaka  2009 akitokea Inter Milan hadi sasa ameweza kushinda makombe matatu akiwa na Man city ambayo ni kombe la ligi (2012), FA cup (2011) na Community shiled (2012). 

Awkward: Mancini shakes hands with City chief Ferran Soriano as chairman Khaldoon Al Mubarak (right) watches
Roberto Mancini akisalimiana na uongozi wa Man city baada ya mechi ya fainali dhidi ya Wigan kumalizika ndani uwanja wa Wembley (Kulia ni bwana Khaldoon Al Mubarak mmiliki wa Man city) 
Lonely: The Italian collects his runners-up medal after the shock defeat by Wigan
Mancini akikatisha mbele ya umati wa watu akiwa ameangalia chini kwa aibu baada ya Man city kufungwa na Wigan katika mchezo wa fainali za FA cup. 
Coming in? Reports suggest Manuel Pellegrini is set to take over Mancini at the end of the season
Pellegrini kocha mkuu wa Malaga anayetarajiwa kuchukua mikoba ya Mancini hivi karibuni

No comments:

Post a Comment