Tuesday, January 28, 2014

Video mpya: Goli la Maradona alilowafunga England

Video hii ni mpya ya Diego Maradona iliyotoka hivi karibuni kutoka kwenye maktaba ya mtu mmoja huko nchini Mexico. Video hii imeshaenea kwa kasi kwenye mitandao mbalimbali duniani zikiwemo TV za michezo ikionesha kiwango kikubwa cha Diego Maradona siku alipofunga goli kwenye michuano ya kombe la dunia iliyofanyika nchini Mexico mwaka 1986. Maradona alifunga goli hili akiwa na timu yake ya taifa Argentina dhidi ya England. Wachambuzi wengi wa soka wamelisifia goli hili na kusema ni moja kati ya magoli bora kufungwa kwenye historia ya soka duniani. Bofya kuangalia kipaji alichokuwa nacho Diego Maradona 'baba wa mpira nchini Argentina'

No comments:

Post a Comment