Wednesday, March 27, 2013

Ibrahimovic huru kucheza mechi ya Barcelona - UEFA


UEFA wamepunguza adhabu ya mshambuliaji wa PSG Ibrahimovic baada ya kupata kadi mbili za njano katika mechi kati ya Valencia na PSG. Ibrahimovic alikuwa amepewa adhabu ya kutocheza mechi mbili lakini UEFA imepunguza na kubakiza mechi moja, mechi ambayo alishaadhibikia kati ya PSG na Valencia. Kwahivyo Ibrahimovic atacheza mechi zote mbili kati ya PSG na Barcelona mwezi ujao. Ibrahimovic ndiye mfungaji tegemezi wa PSG uwepo wake kwenye mechi muhimu kama ya Barcelona ni nguvu tosha kwa PSG kufanikisha ushindi ikizingatiwa ni mchezaji mrefu na mwenye nguvu ya kutetemesha mabeki wa Barcelona. 

No comments:

Post a Comment