Friday, April 12, 2013

Nyoni na wenzake wamesharipoti kuikabili Simba

Wachezaji wanne wa Azam FC waliosimamishwa kupisha uchunguzi wa tuhuma za rushwa dhidi yao wameripoti kambini tayari kuikabili Simba SC siku ya jumapili. Wachezaji hao ni Moradi, Nyoni, Aggrey na Dida, kurejea kwa wachezaji hao kunamaliza mgogoro uliokuwepo na Azam ambao ulidumu kwa takribani miezi mitano. Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya TAKUKURU kuchunguza tuhuma hizo na kuthibitisha kuwa wachezaji hao hawaja husika na rushwa dhidi ya club ya Simba. Wachezaji hao wanatarajiwa kuwemo kwenye mchezo wa Jumapili dhidi ya Simba SC ikiwa ni mchezo muhimu sana kwa Azam FC kwani ikishinda itaizidi Simba SC pointi 14 huku Simba ikisaliwa na michezo minne na hivyo kumaanisha kuwa Kagera Sugar atabaki kuwa mpinzani pekee wa Azam FC katika kuwania nafasi ya pili.

No comments:

Post a Comment