Friday, April 12, 2013

Wilshere na Walcott wamerudi kuikabili Norwich

Wachezaji wa Arsenal akiwemo Jack Wilshere na Theo Walcott  wakifanya mazoezi leo asubuhi. Wilshere na Walcott walikuwa majeruhi kwa kipindi cha mwezi mmoja wanatarajiwa kuwepo kwenye mechi ya jumamosi dhidi ya Norwich. Wilshere ambaye hajacheza tokea March 3 alikuwa anasumbuliwa na kifundo cha mguu wakati Walcott alikuwa anasumbuliwa na maumivu ya paja. Kurudi kwa Walcott na Wilshere kutaipa nguvu Arsenal katika mbio zake za kuwania nafasi ya ushiriki club bingwa ulaya (UEFA champions)

No comments:

Post a Comment