Mashabiki wa klabu ya Simba
wamesema wanaimani na chipukizi wao kuwa watawafunga Yanga katika mchezo wa
mwisho wa ligi kuu Tanzania bara utakaofanyika tarehe 18 mwezi Mei. Mashabiki
hao wamesema wanauhakika na ushindi dhidi ya Yanga, kwani nia yao ni kuondoa
utamu wa kutwaa kombe la ligi kwa vile
wanajua siku ya tarehe 18 baada ya mechi ndipo Yanga
atakabidhiwa kombe hivyo kama Yanga atafungwa na Simba kwenye huo mchezo basi
raha ya kushangilia itakuwa imeingia dosari, lakini mchezaji
wa zamani wa Simba Zamoyoni Mogella amesema chipukizi hao wa Simba wataweza kufanya
maajabu hayo kama wataweza kutumia vyema kipindi cha kwanza ili wajipatie magoli ya
kutosha mapema bila kuchelewa hadi kipindi cha pili ambapo huwa wanachoka na
kuwapa mwanya wapinzani wao. Simba inayoshikilia nafasi ya tatu kwenye msimamo
wa ligi kwasasa imeamua kuwapa nafasi chipukizi wake kuonesha uwezo wao lakini
vilevile kuwajenga ili waje kuchukua nafasi kwenye kikosi cha kwanza, chipukizi
hao wamekuwa wakicheza mechi kadhaa za mwisho wa ligi na wanatarajiwa kushuka
dimbani tarehe 18 dhidi ya Yanga.
No comments:
Post a Comment